Wednesday, May 29, 2013

WAENDESHA PIKIPIKI WATAKIWA KUJIUNGA NA VYUO VYA UDEREVA

Mkuu wa mkoa wa KAGERA, Kanali Mstaafu FABIAN MASSAWE amewataka waendesha PIKIPIKI  kuachana na  tabia ya kuendesha PIKIPIKI  kwa  mazoea badala yake wajiunge na vyuo vinavyotoa mafunzo ya udereva ili waweze kuelewa vyema kanuni na sheria zinazohusiana na masuala ya usalama barabarani hali ambayo  itakayopunguza ongezeko la ajali mkoani humo.
 
Kanali MASSAWE ametoa kauli hiyo wakati akiitimisha mafunzo wa mwezi mmoja yaliyoandaliwa na chuo cha udereva cha LAKE ZONE kilichoko mjini BUKOBA yaliyotolewa kwa waendesha vyombo vya moto  wa kijiji cha BUGANGO kilichoko wilayani MISSENYI.
 
MASSAWE amewaambia  madereva wanaoendesha PIKIPIKI  zinazofanya biashara ya kubeba abiria maarufu kwa jina la BODA BODA wazingatie sheria iliyowekewa ya kuvaa kofia ngumu , amesema anayeendesha pikipiki bila kuvaa kofia ni sawa na mtu anayedhamilia kujinyonga.
 

Mwenyekiti wa kamati ya usalama barabarani mkoani KAGERA ambaye pia ni Mkurugenzi wa chuo cha udereva cha LAKE ZONE, WINSTON KABANTEGA, amemweleza mkuu wa mkoa kuwa mwamko wa waendesha pikipiki wa kuhudhuria mafunzo ya udereva imewajengea uwezo mkubwa na hivyo wanaendesha pikipiki kwa kujiamini na bila woga.
 

Kwa upande wake afisa wa kikosi cha usalama barabarani, PETER MAGAYANE, amesema ajali mkoani KAGERA zinapungua kwa kasi, amesema kupungua kwa ajali hizo kunachangiwa hatua  idadi kubwa ya waendesha vyombo ya kuchukua uamzi wa kuhudhuria mafunzo ya udereva, amesema ajali chache zinazotokea mkoani kagera zinachangiwa na mambo anayoyabanisha.
 

Nao baadhi ya wahitimu wa mafunzo hayo kwa nyakati tofauti wameahidi kuzingatia mafunzo waliyoyapata ili waweze kujiepusha na ajali, wamesema kuwa mafunzo hayo yamewawezesha kuelewa vizuri kanuni na sheria za usalama barabarani.
 



No comments:

Post a Comment