Wednesday, May 22, 2013

MKUU WA MKOA KAGERA AZINDUA MASHINDANO YA UMISETA



Wanafunzi Wakiwa Kwenye Maandamano Kuelekea Kwenye Uzinduzi wa Michezo ya UMISSETA Mkoani Kagera

Mkuu wa Mkoa Kagera na Wageni Wengine Wakipokea Maandamano ya Wanamichezo Wanafunzi Chuoni Katoke Wilayani Muleba.


 
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Kanali Mstaafu Fabiani I. Massawe amezindua rasmi mashindano ya UMISSETA (Umoja wa Michezo Shule za Sekondari Tanzania) mkoani Kagera katika Chuo cha Ualimu Katoke Wilayani Muleba.

Uzinduzi wa mashindano ya UMISSETA mkoani Kagera ni maandalizi ya kushindanisha na kubaini vipaji mbalimbali  katika michezo na kuunda timu ya mkoa wa Kagera itakayokwenda kushriki katika ngazi ya Kanda mpaka taifa.
Mhe. Massawe akizindua michezo hiyo alisistiza wanafunzi hao kuwa na nidhamu wakati wote wa mashindano hayo pia na kucheza kwa mshikamano ili kuonesha vipaji  vyao na kupitia huko waweze kupata ajira kama wanamichezo maarufu wengi walivyo duniani.
Pia Mhe. Massawe aliagiza viongozi wote mkoani Kagera kuipa kipaumbele michezo na aliwaagiza viongozi wote wa kisiasa kuipa sana msukumo mkubwa michezo ili mkoa wa Kagera uweze kutoa vipaji kwa wingi na kutengeneza nafasi za ajira kwa vijana.
Aidha, Mkuu wa Mkoa alitoa rai ya michezo mingine kuangaliwa na kupewa kipaumbele kuliko kuendelea kusistiza aina fulani ya michezo. “Mwaka kesho ningependa kuona michezo ya maigizo, nyimbo na ngoma za kitamaduni , michezo hiyo nayo ipewe kipaumbele.” Alisitiza Mhe. Massawe.
Mashindano ya UMISSETA mkoani Kagera yanashirikisha wanafunzi wa shule za Sekondari kutoka katika Halmashauri za Wilaya za Missenyi, Karagwe, Ngara, Biharamulo, Muleba, Bukoba na Manispaa ya Bukoba.
Jumla ya wanafunzi wa shule za sekondari wanaoshiriki katika mashindano ya UMISSETA mkoani Kagera ni 568, wanafunzi wa kiume 301 na wanafunzi wa kike 267. Wananfunzi hao  wanashiriki michezo ya mpira Wa miguu, mpira wa mikono, riadha, mpira wa wavu, kuruka na kurusha tufe.
Imeandaliwa na:
Sylvester Raphael
AFISA HABARI
RS-KAGERA@2013


No comments:

Post a Comment