Thursday, February 27, 2014

MAZISHI YA MWALIMU EMMANUEL RWETOIJELA

 Familia ya Revelian Mwesiga ilikuwa miongoni mwa walioudhuria mazishi ya mwalimu Emmanuel Rwetoijela yaliyofanyika katika kijiji cha Rwangono.
 Mzee Sosi Rushaka na Mwassa nao walioudhuria mazishi hayo.
 Baadhi ya watoto wa marehemu Rwetoijela.

RAIS KIKWETE AZINDUA MTAMBO WA KUHAKIKI TAKWIMU ZA SIMU ZA KIMATAIFA

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe kuzindua rasmi Mtambo wa Kuhakiki Takwimu za Mawasiliano (Telecommunication Traffic Monitoring System) leo February 27, 2014 katika jengo la Mawasiliano Towers jijini Dar es salaam. Kulia ni Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Pro, Makame Mnyaa Mbarawa, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt Fenella Mukangara, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Prof. John Nkoma, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Saidi Meck Sadick na wadau wengine wa tehama
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akibofya kitufe  kuzindua rasmi Mtambo wa Kuhakiki Takwimu za Mawasiliano (Telecommunication Traffic Monitoring System) leo February 27, 2014 katika jengo la Mawasiliano Towers jijini Dar es salaam.
t3: t1: Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata maelezo ya  Mtambo wa Kuhakiki Takwimu za Mawasiliano (Telecommunication Traffic Monitoring System) aliouzindua leo February 27, 2014 katika jengo la Mawasiliano Towers jijini Dar es salaam. Kulia ni Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Pro, Makame Mnyaa Mbarawa, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt Fenella Mukangara, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Prof. John Nkoma, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Saidi Meck Sadick na wadau wengine wa tehama.
PICHA NA IKULU

MAMBO YA BUNGE LA KATIBA

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Spika wa Bunge, Anne Makinda kwenye ukumbi wa  Bunge mjini Dodoma katika semina  ya Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Februari 27, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma Februari 27, 2014. Kutoka kushoto ni Maria Sarungi, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Mahusiano na Uratibu na Mbunge wa Bunda, Stephen Wasira na Mbunge wa Igalula,Athumani, Mfutakamba. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Wednesday, February 26, 2014

Waziri mkuu Pinda Rais wa kampuni ya Schlumberger

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na  Rais  wa  kampuni ya  Schlumberger Kanda ya Afrika na Ulaya, Bibi  Catherine MacGregor kabla ya mazungumzo yao,  kwenye makazi ya Waziri Mkuu, mjini Dodoma Februari  26,2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

MJUMBE WA BARAZA LA ARDHI KASAMBYA KIKAANGONI

MJUMBE wa baraza la ardhi la  kata Kasambya katika wilaya ya Misenyi Egidius Medard amehukumiwa na mahakama kwenda jela kutumia kifungo cha miaka mitatu au kulipa faini ya shilingi 500,000 baada ya mahakama huyo kuthibitisha tuhuma zilizokuwa zinamkabili.

Hukumu hiyo imetolewa  hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama  ya Bukoba, Sylivia Lushasi jana baada ya mahakama hiyo kuridhika na ushahidi uliotolewa na upande na mlalamikaji ulioongozwa taasisi ya kupambana na rushwa (TAKUKURU) mkoani Kagera.

 Tuhuma iliyomtia hatiani Medard ni ya kuomba na kupokea rushwa ya shilingi 200,000 toka kwa Haulat Mohamed ambaye alikuwa na mgogoro wa masuala ya ardhi na jirani yake ili ziweze kuwashawishi wajumbe wa baraza la ardhi waweze kutoa hukumu ya upendeleo kwa upande wake.

Mheshimiwa Lushasi alisema mahakama imetoa hukumu hiyo ili iwe fundisho kwa wajumbe wa mabaraza ya ardhi ya kata wanaotoa hukumu kwa upendeleo kwa ushawishi wa fedha na mali nyingine.

Amesema vitendo vinavyofanywa na baadhi ya wajumbe wa mabaraza ya ardhi vya kuomba rushwa ili vipindishe hukumu kuwa kamwe havitavumiliwa, hakimu huyo amesema vinawanyima haki baadhi ya watu wamaostahili kupata zao.

Mheshimiwa Lushasi amemaliza kwa kusema hata vitendo vya watu kujichukulia sheria mikononi vinavyojitokeza ndani ya jamii kwa kiasi fulani vinachangiwa na baadhi ya waliopewa mamlaka ya kusimamia amani ambao wanafanya kazi kinyume na taratibu zinazowaongoza.

Mwendesha mashtaka wa TAKUKURU Fortunatus Mpangamila, awali alisema kuwa Medard alikamatwa na maofisa wa taasisi hiyo julai 5, 2011 akiwa kwenye harakati za kupokea kiasi cha shilingi 200,000, alisema maofisa hao walimnasa Medard baada ya kumuwekea mtego.

Hata hivyo Medard alipelekwa gerezani baada kukosa faini ya shilingi 500, 000 ambayo alipaswa kuitoa kama adhabu hivyo atatumikia kifungo cha miaka mitatu gerezani.

WAZIRI MKUU BUNGENI DODOMA

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na wabunge wa Bunge Maalum la Katiba nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma, Februari 25, 2014. Kutoka kushoto ni Abdallh Sharia  Ameir, Riziki Said Lulida na  Jerome Dismas Bwausi.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Monday, February 24, 2014

SHEREHE YA UZINDUZI WA MAHAKAMA YA RUFAA YA MAHAKAMA KUU KANDA YA BUKOBA

 Baadhi ya majiji walioudhuria ufunguzi wa mahakama rufaa ya mahakama kuu kanda ya Bukoba uliofanywa na jaji mkuu Othman Chande.
 Baadhi ya maofisa wa serikali, kushoto ni katibu tawala wa mkoa wa Kagera, Nassor Mnambila.
 Baadhi ya walioudhuria sherehe hiyo,kulia ni mkuu wa wilaya ya Bukoba, Bi Ziporah Pangani.
 Bw. Kadushi Mwanasheria wa serikali.
 Baadhi ya mawakili wa serikali na mawakili wa kujitegemea.

Mh.Jaji Luanda akiteta jambo na majaji wenzake.

MAMBO YA BUNGE LA KATIBA

 



  Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na  Mbunge wa Bunge Maalum la Katiba na Mbunge wa Zamani wa Morogoro, Shamim Khan, nje ya  ukumbi wa Bunge mjini Dodoma  Februari 24, 2014. Kulia ni mbunge wa Sumve Richard Ndassa. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
  Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mbunge wa Singida Magharibi Mohamed Bissanga na Mbunge wa Sumve, Richard Ndassa ,wote wakiwa ni wabunge wa Bunge  Maalum la Katiba, nje ya ukumbi wa Bunge Mjiji Dodoama Februari 24, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


Sunday, February 23, 2014

KILELE CHA MAADHIMISHO YA BONDE LA MTO NILE

 Mkuu wa wilaya ya Bukoba Bi. Ziporah Pangani akiongea wakati wa zoezi la upandaji wa miti uliofanyika katika shule ya msingi ya Mugeza mseto.
 Katibu tawala wa mkoa wa Kagera, Nassor Mnambila.





Mkuu wa mkoa wa Kagera, kanali Mstaafu Fabian Massawe akishiriki kwenye zoezi la upandaji wa miti.

HARAMBEE YA KUCHANGIA UJENZI YA WODI YA WATOTO MUHIMBILI

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Marais wastaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi na Mzee Benjmin William Mkapa baada ya kuwasili katika hafla ya harambee ya kuchangia ujenzi wa wodi ya dharura kwa watoto pamoja na vifaa vyake katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Kati ya kiasi cha shilingi 1bn/ zilizohitajika, jumla ya shilingi 602,080,000/- zilipatikana katika harambee hiyo iliyofanyika usiku wa Jumamosi Fabruari 22, 2014 katika hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es salaam.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akibadilishana mawazo  na Marais wastaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi na Mzee Benjmin William Mkapa katika hafla ya harambee ya kuchangia ujenzi wa wodi ya dharura kwa watoto pamoja na vifaa vyake katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Kati ya kiasi cha shilingi 1bn/ zilizohitajika, jumla ya shilingi 602,080,000/- zilipatikana katika harambee hiyo iliyofanyika usiku wa Jumamosi Fabruari 22, 2014 katika hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es salaam.

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimshukuru mwakilishi wa UNICEF nchini kwa mchango wa dola za kimarekani 100,000 huku  Marais wastaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi na Mzee Benjmin William Mkapa wakishuhudia katika  hafla ya harambee ya kuchangia ujenzi wa wodi ya dharura kwa watoto pamoja na vifaa vyake katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Kati ya kiasi cha shilingi 1bn/ zilizohitajika, jumla ya shilingi 602,080,000/- zilipatikana katika harambee hiyo iliyofanyika usiku wa Jumamosi Fabruari 22, 2014 katika hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es salaam.





WAZIRI MKUU PINDA AHUTUBIA SEMINA YA WATENDAJI WA JUMUIA YA WAZAZI CCM


 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akihutubia semina ya viongozi na  watendaji  wa Jumuiya  ya Wazazi  Ngazi ya Taifa, mikoa na Wilaya nchini iliyofanyika kwenye ukumbi wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM mjini Dodoma Februari  22, 2014wakimsikiliza Waziri Mkuu, Mizengo Pinda wakati alipofungua semiana hiyo. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

 Washiriki wa Semina ya viongozi na  watendaji  wa Jumuiya  ya Wazazi  Ngazi ya Taifa,mikoa na Wilaya nchini iliyofanyika kwenye ukumbi wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM mjini Dodoma Februari  22, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiongozana na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Tanzania,Abdallah Majura Bulembo  (kulia)  na Makamu wake  Dogo Idd Mabrouk (Wapili kushoto) na Mjumbe wa Kamati yaUtekelezaji ya Jumuiya hiyo,Mohammed Sif Khatib (wapili kulia) kutoka kwenye ukumbi wa Halmashauri Kuu ya  Taifa ya CCM mjini Dodoma baada ya kufungua semina  viongozi na  watendaji  wa Jumuiya  ya Wazazi  Ngazi ya Taifa,mikoa na Wilaya nchini ,Februari  22, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)



Thursday, February 20, 2014

MKUU WA MKOA KAGERA ATEMBELEA MWALO WA KASTAMU



Mkuu wa mkoa wa Kagera, Kanali Mstaafu Fabian Massawe akiangalia samaki aina ya Mboju alipotembelea mwalo wa Kastamu kukagua hali ya usafi, samaki hao adimu  wako kwenye hatari ya kutoweka ikiwa wavuvi wataendelea kutumia zana haramu za uvuvi ndani ya ziwa Victoria, mkuu huyo aliwaambia wavuvi katika mwalo huo kutumia zana bora za uvivi ili walinde rasilimali zinazopatikana katia ziwa hilo.
Huyu ndiye samaki aina ya Mboju wanaopatikana ndani ya ziwa victoria,, huuzwa kwa bei ya wasztani kati ya shilingi 15,000 hadi 50,000 kwa mmoja.
Baadhi ya wafanyabiashara wa eneo la mwalo wa nyamkazi.

Massawe akikagua usafi eneo la Buyekela.