Wednesday, March 27, 2013

WIMBO WA KUHAMASISHA KASI YA MAENDELEO WAZINDULIWA KAGERA

MKOA wa Kagera umezindua wimbo maalumu utakaokuwa ukiimbwa wakati wa shughuli mbalimbali za kuhamasisha masuala ya maendeleo na  amani mkoani humo ambao umetungwa na msanii maarufu hapa nchini mwalimu John Mgango.

Wimbo huo umezinduliwa rasmi jana na mkuu wa mkoa wa Kagera Kanali Mstaafu Fabiani Massawe wakati wa kikao cha ushauri cha mkoa wa Kagera (RCC) kilichokuwa na lengo la kupitisha mapendekezo ya bajeti ya mwaka wa fedha 2013/14 kilichofanyika kwenye ukumbi wa mkuu wa mkoa huyo uliko katika manispaa ya Bukoba.

Akizundua wimbo huo awaagiza viongozi wahakikishe wimbo unahubiliwa  kwa kuwa utasaidia kuwaelimisha wanachi kuelewa mambo yanayokwamisha  maendele mkoani humo  na yanayochangia uvunjifu wa amani.

Mkuu huyo wa mkoa ameendelea kusema kuwa wimbo huo ulitafutiwa maneno mazuri yanayolenga dhana halisi ya amani na maendeleo ya mkoa wa Kagera, amesema mkoa wa Kagera una mkakati mkubwa wa kutokomeza vitendo vinavyokwamisha maendeleo na uvunjifu wa amani.


Kwa upande wake mtunzi wa wimbo huo John Mgango wakati wa uzinduzi huo amewaomba Watanzania wajiepushe na mkifarakano ili waweze kudumisha amani hapa nchini .

Massawe ni mmoja wa wanaharakati wa masuala ya maendeleo hapa nchini, mkoani Kagera amefanikiwa kubadili ya  mkitazamo ya wananchi mkoani humo hali ambayo imewawezesha kuondokana na masuala ya uvivu, majungu na masuala mengine yaliyokuwa yanakwamisha maendeleo mkoani Kagera.

No comments:

Post a Comment