Tuesday, January 29, 2013

TAHADHALI YA MVUA KUBW KWENYE MAENEOMENGI TANZANIA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA UCHUKUZI
MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA
Simu: 255 22 2460735/2460706
FAKSI: 255 22 2460735/2460700 S.L.P. 3056
Simu pepe: met@meteo.go.tz DAR ES SALAAM
Tovuti: www.meteo.go.tz
Unapojibu tafadhali nakili:
Kumb. Na.: TMA/1622 29 Januari, 2013
Taarifa kwa umma: Uwezekano wa matukio ya mvua kubwa
Taarifa Na. 20130129-02
Muda wa Kutolewa
Saa za Afrika Mashariki
Saa 12:00 Jioni
Daraja la Taarifa:
1:Taarifa 2:Ushauri
3:Tahadhari
4:Tahadhari Kubwa:
Ushauri
Kuanzia:
Tarehe
30 Januari, 2013
Mpaka:
Tarehe
01 Februari, 2013
Aina ya Tukio Linalotarajiwa
Mvua kubwa (zaidi ya milimita 50 katika kipindi cha saa 24 kila
siku)
Kiwango cha uhakika: Wastani
Maeneo yatakayoathirika
Baadhi ya maeneo ya mikoa ya Rukwa, Iringa, Mbeya, Njombe,
Ruvuma, Morogoro, Lindi, Pwani, Mtwara na maeneo jirani na
mikoa hiyo.
Maelezo:
Kuwepo kwa kimbunga “FELLENG” kaskazini-mashariki mwa
Madagascar ambacho kinavuta upepo wenye unyevunyevu
kutoka Congo kupitia maeneo tajwa hapo juu.
Angalizo:
Wakazi wa maeneo hatarishi, watumiaji wa Bahari na nchi kavu
wanashauriwa kuchukua tahadhari. Aidha taasisi zinazohusika
na Maafa zinashauriwa kuchukua hatua stahiki.
Maelezo ya Ziada
Mamlaka inaendelea kufuatilia mwenendo wa kimbunga hicho
na kutoa mrejeo (updates) kila itakapobidi.
IMETOLEWA NA MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA

No comments:

Post a Comment