Wednesday, January 23, 2013

MANGULA ASHINDWA KUMNUSURU MEYA WA MANISPAA YA BUKOBA ANATORY AMANI, MKAKATI WA KUMUENGUA WABAKIA PALEPALE

MAKAMU Mwenyekiti  wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Philip Mangula ameshindwa kumunusuru Meya wa manispaa ya Bukoba, Anatory Amani asienguliwe na madiwani wanaotaka kumpigia kura za kutokuwa na imani naye kulingana na utendaji wake wa kazi.

Pamoja na ushawishi mkubwa alioufanyaMangula wa kutaka kumnusuru Meya huyo  madiwani hao wameonekana kushirikia msimamo wao wa kutaka Meya huyo aachie ngazi.

Madiwani hao walionyesha msimamo wao wakati wa kikao cha dharula cha halmashauri ya kuu ya Bukoba kilichofanyika kwenye ukumbi wa mtakakatifu Francis uliko katika manispaa ya Bukoba.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotoka ndani ya kikao hicho kilichomalizika majira ya saa 9.00 leo baadhi ya madiwani  na wajumbe wa halmashauri kuu ya Bukoba  walimkataa waziwazi  Mstahiki meya Amani kwa kuonyesha vielelezo mbele ya Philip Mangula.

Wajumbe wa halmashauri hiyo kuu walikataa uamzi wa Philip Mangula aliyetaka tume maalumu iundwe ya kuchunguza tuhuma zinazomkabili mstahiki Meya huyo.

Walimweleza Mangula kuwa kama anataka kuunda tume ya kuchinguza tuhuma zinazomkabili Amani kuwa ni lazima ahakikishe Meya huyo anaachia ofisi ili apishe uchunguzi.

Baadhi ya wajumbe wa kikao hicho walimweleza Mangula kuwa mambo anayoyafanya yanalenga kuifilisi Halmashauri ya manispaa ya Bukoba, kwa nyakati tofauti wameonyesha kutoridhishwa na matumizi ya mamilioni ya pesa yanayofanywa na meya huyo na mikataba  ya miradi anayoibuni katika manispaa hiyo.

Wamemweleza Mangula kuwa hawamtakio Meya huyo na ndio maana wanataka kumpigia kura za kutokuwa na imani naye, katika hali isiyo ya kawaida madiwani hao walikataa kutii maelekezo yaliyotolewa Mangula.

Mangula aliwataka madiwani wote 8 wa CCM  waliosaini waraka wa kutaka Meya apigiwe kura za kutokuwa na imani naye waondoe saini zao kwenye waraka huo la sivyo wangenyanganywa uanachama, madiwani hao walikataa maelekezo hayo.

Mangula aliwatishia madiwani hao kuwa madiwani ambao walisaini waraka huo ambao wangekataa kuondoa saini zao kuwa chama hicho kingewanyanganya kadi za uanachama.

Habari ambazo gazetib hili limezipata ni kwamba mchakato wa kikao cha baraza la madiwani kitakachojadili hatima ya Mstahiki Meya Amani  kitafanyika januari, 28 mwaka huu.

Meya huyo anakabiliwa na tuhuma ya kuingia mikataba mibovu wa miradi ya ujenzi wa soko kuu la Bukoba, upimaji wa viwanja, ujenzi wa jengo la kitega uchumi, Meya huyo amekuwa akituhumiwa kwa kufanya mambo kwa usiri mkubwa.

1 comment:

  1. amani si uachie ngazi mbona unagangania madaraka kama amin

    ReplyDelete