Monday, March 25, 2013

MANISPAA YA BUKOBA MAMBO YAENDELEA KUWAKA MOTO

BAADHI ya madiwani wa halmashauri ya manispaa ya Bukoba wamegomea kikao cha baraza hilo na kutoka nje ya ukumbi wa mkutano baada ya kutokea malumbano makali kati yao na  mstahiki Meya wa manispaa hiyo Anatory Amani.


Hicho kilikuwa kikao cha kawaida cha baraza la madiwani wa manispaa hiyo cha kujadili masuala ya mbalimbali yakiwemo ya  utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kupokea taarifa za kamati, kilifanyika kwenye ukumbi wa halmashauri ya manispaa hiyo.


Mgogoro  ulianza baada ya madiwani  kuanza kuhoji  baadhi ya vipengele vya muhtasari wa kikao cha baraza la madiwani kilichopita kabla ya kuuthibitisha, wamedai kwamba katika kikao hicho kilichopita kuwa hawakukubaliana kurasimisha madaraka kwa kamati ya fedha na uchumi ili ifanye mchakato wa  kukopa fedha zaidi ya shilingi milioni 450 kwa ajili ya  kuwalipa wadeni.


Wakizungumza kwa nyakati tofauti  madiwani hao wamesema katika kikao kilichopita hawakutoa Baraka kwa kamati ya fedha na uchumi kufanya mchakato kukopa fedha zaidi ya shjlingi milioni 200 toka  benki ya rasilimali nchini (TIB) kwa ajili ya kuilipa kampuni ya OGM itakayosimamia ujenzi wa soko jipya la Bukoba  na shilingi zaidi ya milioni 250 kwa ajili ya ajili ya kuandaa maeneo mbadala yatakayotumiwa wafanyabiashara watakaopisha ujenzi wa soko jipya la Bukoba. .


Madiwani wa halmashauri ya manispaa ya Bukoba kila mara wamekuwa wakidai kuwa hawana imani na Meya Amani, kila mara wamekuwa wakimtaka aachachie ngazi kufuatia tuhuma mbalimbali wanazozielekeza kwake, madiwani wanamtuhumu diwani kuwa anaingia mikataba ya miradi mbalimbali ya maendeleo kinyemela, miradi anayodai meya ameiingia kinyemela kuwa ni pamoja na ujenzi wa soko jipya la Bukoba, upimaji wa viwanja 5,000 na ujenzi wa standi kuu ya mabasi.

No comments:

Post a Comment