Tuesday, March 05, 2013

Matokeo ya mwanzo ya uchaguzi Kenya



Wapiga kura kwenye foleni

Matokeo ya mwanzoya uchaguzi mkuu nchini Kenya yanaonyesha Uhuru Kenyatta akiwa anaongoza kwa asilimia hamsini na nne dhidi ya Raila Odinga aliye na asilimia arobaini na moja.
Ni uchaguzi ambao mamilioni ya wakenya walishiriki kupiga kura licha ya visa vya vurugu kuripotiwa katika baadhi ya sehemu za nchi ambapo takriban watu 15 wakiwemo polisi waliuawa .
Wakenya walisubiri kwa zaidi ya saa nane kupiga kura ikizingatiwa kuwa baadhi walikuwa katika vituo vya kupigia kura mapema asubuhi saa za tisa na hata saa nane wakisubiri vituo kufunguliwa.
Mamilioni ya wakenya wanatumai kuwa matokeo ya uchaguzi huu yatawaunganisha wananchi hasa baada ya ghasia kushuhudiwa baada ya uchaguzi wa mwaka 2007. Watu elfu moja na miambili waliuawa na maelfu ya wengine kuachwa bila makao.
Matokeo ya mwanzo yanaonyesha Uhuru akiongoza kwa zaidi ya asilimia hamsini dhidi ya mpinzani wake Raila Odinga, 68.
Tume ya uchaguzi inasema kuwa shughuli ya kuhesabu kura huenda ikaendelea hadi Jumatano kwa sababu ya idadi kubwa ya wapiga kura walioshiriki zoezi hilo.
Hatua hii nayo huenda ikachelewesha kutangaza matokeo rasmi ya uchaguzi mkuu.
Watu waliendesha shughuli hiyo kwa amani kwani ndiyo ilikuwa kauli mbiu ya uchaguzi huu kwa hofu ya kutokea tena ghasia za kikabila zilizoshuhudiwa mwaka 2007.


No comments:

Post a Comment