Baadhi ya wanafunzi wakiandamana.
 Wanafunzi wa kidato cha sita na cha tano wakiwa nje ya jengo la manispaa ya Bukoba.
 Mkuu wa wilaya ya Bukoba Bi Ziporah Lion Pangani akiongea na wanafunzi shule ya sekondari ya Ihungo waliofanya maandamano.
 Wanafunzi wakisikiliza kwa makini.
WANAFUNZI wa kidato cha tano na sita wa shule ya sekondari Ihungo ambayo
 ni miongoni mwa shule kongwe hapa nchini iliyoko katika manispaa ya 
Bukoba wameandamana hadi kwenye ofisi ya mkuu wa wilaya ya Bukoba 
kupinga vitendo wanavyofanyiwa na baadhi ya walimu wao.
Wanafunzi hao waliandamana jana  hadi kwenye ofisi ya mkuu wa wilaya
 ya Bukoba Ziporah Pangani na kutoa malalamiko mbele yake kwa kile 
walichodai kuwa wanafanyiwa hujuma na mwalimu anayewafundisha somo la 
kemia waliyemtaja kwa jina la Philemon Tumwesige.
Kwa nyakati tofauti bila kutaja majina yao wakimlalamikia mwalimu 
Tumwesige walisema kuwa amekuwa ha tabia ya kutoingia darasani 
kuwafundisha somo hilo la kemia, walisema kuwa tangu mwaka huu wa sasa 
wa masomo uanze ameingia darasani mara 13  wakati katika kipindi hicho 
alitakiwa kuwa ameingia darasani mara 56.
Waliendelea kumlalamikia kwa kumueleza mkuu wa wilaya kuwa amekuwa 
na tabia ya kuwachangisha fedha ili aweze kuwafundisha, walisema mwalimu
 Tumwesige alikuwa akimtaka kila mwanafunzi amchangie shilingi 5,000 ili
 aweze kuingia darasani.
Walisema idadi kubwa wanafunzi walimchangia kiasi hicho, walimweleza
 mkuu huyo wa wilaya kuwa pamoja na kumchangia kiasi hicho cha fedha 
amekuwa akigoma kuwafundisha na mara kwa mara alikuwa akisema kuwa 
anafanya hivyo ili wanafunzi wa shule hiyo wasifaulu somo la kemia.
Wanafunzi hao walisema kinachodhihirisha mkakati wake wa kutaka 
wanafunzi wasifaulu mtihani wao wa kemia ni matokea ya mtihani wa 
majaribio wa somo la kemia uliofanywa na wanafunzi wa kidato cha sita 
katika shule hiyo, walisema kati ya wanafunzi zaidi ya 400 wa kidato cha
 sita waliofanya somo hilo la  kemia waliofaulu ni 17 tu.
Walimuomba mkuu wa wilaya afanye utaratibu ili wapatiwe mwalimu 
mwingine wa kemia, walisema kamwe mwalimu huyo awezi kuwapa elimu sahihi
 kwa kuwa wameishavutana naye sana, walisema kila siku wamekuwa 
wakimtolea taarifa kwa uongozi wa juu wa shule hiyo lakini hatua 
zimekuwa hazichukuliwi dhidi yake.
Mkuu wa wilaya Bi. Pangani aliwaahidi kushughulikia suala hilo 
haraka iwezekanavyo ili lipatiwe ufumbuzi, aliwaambia warudi shuleni 
watulie ili ofisi ya elimu iweze kushughulikia suala hilo, "Nendeni 
shuleni mtulie najua mnadai haki yetu na haki yenu itapatikana. 
Alimaliza.
 





 
No comments:
Post a Comment