Monday, December 16, 2013

TAARIFA YA KUTATUA MGOGORO YAHAIRISHWA

Mkaguzi wa hesabu za serikali ameahirisha kwa muda kutoa taarifa ya juu tuhuma ya matumizi mabaya ya madaraka iliyokuwa imeelekezwa kwa mstahiki Meya wa manispaa ya Bukoba, Khamis Kagasheki iliyoelekezwa kwake na baadhi ya madiwani wanaompinga wanaoongizwa na waziri wa maliasili na utalii, Balozi Khamis Kagasheki.

Mkaguzi huyo wa serikali alikuwa atoe taarifa hiyo desemba 16, mwaka huu, taarifa hiyo ilikuwa itolewe na mkaguzu huyo kwenye ukumbi wa mkuu wa mkoa wa Kagera.

Taarifa za kuhairishwa kwa utolewaji wa taarifa hiyo zilipatikana siku ya jumapili, kabla ya hapo  madiwani wote walikuwa wameishapatiwa barua za kuhudhuria kikao hicho maalumu kilichokuwa kimeandaliwa na ofisi za mkaguzi huyo.

Taarifa zinadai kuwa mkaguzi huyo ameaahirisha zoezi la kutoa taarifa hiyo kufuatia majukumu yaliyomkabili, hata hiyo uamzi wa kuhairisha kikao hicho umewakatisha tamaa baadgi ya wananchi katika manispaa ya Bukoba, wananchi walikuwa na shauku kubwa ya kusikia mgogoro unahitimishwa ili masuala ya maendeleo yaliyokwama katika manispaa hiyo yaendelee kutekelezwa, ambayo ni pamoja na ujenzi wa soko kuu la Bukoba na standi kuu ya mabasi.

Taarifa ambazo zimepatikana zinadai kuwa mkaguzi huyo ameahidi kutoa taarifa wakati wowote bila kueleza taarifa hiyo itatolewa siku gani.

No comments:

Post a Comment