Friday, December 07, 2012

MAADHIMISHO YA KUPINGA UKATILI NA UNYANYASAJI WA KIJINSIA MKOANI KAGERA

 Askari wakiandamana pamoja na wadau wengine kupinga vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia.
 Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Kagera, Philip Kalangi, akimpokea katibu tawala wa mkoa wa Kagera Nassor Mnambila alipowasili kwenye uwanja wa uhuru kuhudhuria maadhimisho ya kupinga vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia mkoani Kagera.
 Ujumbe uliokuwa ukitolewa na waandamanaji.



JUMLA ya makosa ya ukatili wa kijinsia 612 yalitokea kwenye maeneo mbalimbali yaliyoko  mkoa Kagera katika kipindi cha kuanzia kipindi cha mwezi Januari hadi mwezi Novemba, mwaka huu.

Makosa hayo yaliyotokea  yalibainishwa na kamanda wa jeshi la polisi mkoani Kagera Philip Kalangi (kushoto) kwenye taarifa yake aliyoitoa mbele ya katibu tawala wa mkoa wa Kagera Nassor Mnambila wakati maadhimisho ya kupinga ukatili wa kijinsia yaliyofanyika kwenye viwanja vya uhuru vilivyoko katika manispaa ya Bukoba.

Kwenye taarifa hiyo Kalangi aliyataja makosa ya ukatili wa kijinsia kuwa ni pamoja na 306 ya ubakaji, 12 ya kulawiti, 135 ya shambulio na kipigo, 18 ya kutorosha wanafunzi, 96 ya kutelekeza familia, 20 dhidi ya ukatili wa watoto na 25 ya mimba kwa wanafunzi.

Alisema katika kipindi hicho kesi za makosa ya ukatili wa  kijinsia 170 zilifikishwa mahakamani , aliendelea kusema kuwakesi za  makosa 56 bado ziko kwenye upelelezi, kesi za makosa 50 zilipata mafanikio na kesi za makosa 80 zilikosa mafanikio.

Kalangi alisema jeshi la polisi mkoani Kagera litahakikisha linaimarisha amani na utulivu na maendeleo kwa kuchukua hatua mbalimbali dhidi ya wale wote wanaofanya vitendo viovu kwa kushirikiana na wadau wengine wa usalama chini ya dawati la jinsia la jeshi la polisi.

Aliendelea kusema kuwa ukatili na unyanyasaji wa kijinsia ni uharifu kama uharifu mwingine wowote, “jeshi la polisi halitamwonea aibu mtu yotote atakayejihusisha na masuala ya kutekeleza masuala ya ukatili ya kijinsia, tutamshughulikia bila kujali cheo chake, rangi yake na nafasi yake aliyonayo ndani ya jamii” alisema.

Katibu tawala wa mkoa wa Kagera Nassor Mnambila aliyekuwa mgeni rasmi wakati wa maadhimisho hayo alilipongeza jeshi la polisi mkoani humo kwa juhudi linalozifanya za kupambana na vitendo vya uharifu mkoani Kagera.

Alilitaka jeshi hilo lisilegeze kamba badala yake liwashughulikie kikamilifu wale wote wanaijuhusisha na vitendo vunavyohatarisha amani na utulivu ndani ya jamii, alisema serikali mkoani Kagera itaendelea kuliunga mkono jeshi hilo ili likamilishe adhima yake ya kuthibiti kabisa vitendo vya uharifu mkoani Kagera.

No comments:

Post a Comment