NA AUDAX MUTIGANZI
BUKOBA
Jeshi la polisi katika mkoa wa KAGERA limeanza kufanikisha
mikakati yake yenye lengo la kusambaratisha mtandao wa watu wasiojulikana
wanaojihusisha na vitendo vya kufadhili na kufanya mauaji ya kuwakata kata watu
kwa MAPANGA na baadae  kuwanyonya damu
ambavyo  katika kata za KITENDAGULO,
KIBETA na RWAMISHENYE katika manispaa ya BUKOBA.
Katika
 kusambatarisha 
mtandao huo jeshi hilo  limefanikiwa
 kuwaua watuhumiwa WAWILI,  JOHANES JOSEPH  ambaye ni kinara wa mauaji 
ya kuwakata kata
MAPANGA na EDWARD THEOPHIL ambao ni miongoni mwa watuhumiwa  WANNE 
 walioshikiliwa kwa tuhuma ya kuhusika na  kufadhili vitendo mauaji ya 
kuwakata kata
WATU kwa mapanga kwa  ajili ya imani za
KISHIRIKINA.
Akizungumza leo na waandishi wa habari Kamanda wa jeshi la
polisi mkoani KAGERA, HENRY MWAIBAMBE amesema watuhumiwa waliouwawa kwa kutumia
nguvu za giza walikuwa wakijaribu kuwatoroka maofisa wa jeshi la polisi
waliokuwa wakiwahoji wakati wakiwaonyesha 
MAZINDIKO  wanayoyatumia katika
kutekeleza mauaji, pamoja na kutoa onyo kwa wanajihusisha na vitendo hivyo pia
amesema jeshi hilo kwamba linamshikilia   GAUDENSIA NDIBALEMA ambaye ni mganga wa jadi kwa
tuhuma ya kuwapatia kinga wanajihusisha na vitendo vya mauaji hayo.
CLOUDS  TV imefanikiwa
kuongea na baadhi ya wananchi  waliolazwa
 katika 
hospitali ya rufaa ya Mkoa wa KAGERA walioathrikika kufuatia kukithiri
kwa vitendo hivyo, OMARY HABIB na ALCAD MBELWA ni miongoni mwa waathrika wa
vitendo hivyo wanaoeleza walivyovamiwa na wakata mapanga hao na namna
walivyojinusuru, GETRUDO RUBAKULO ni afisa muuguzi ambaye anaeleza hali ya
waathirika hao, huku muuguzi mkuu wa hospitali ya rufaa BEATRICE KABUNGA  takwimu za waliofikishwa hospitalini kwa
kukatwa mapanga katika kipindi cha wiki mbili.
Kufuatia vitendo vya mauaji ya kukata watu kwa mapanga
katika manispaa ya BUKOBA, zaidi ya watu KUMI wameishauwawa , vitendo hivyo
vinahusishwa na imani za kishirikina ambapo inadaiwa kwamba wale wanaokatwa
mapanga damu zao zinavyonywa na kupelekwa pasipojulikana.
For more information contact +255 784 939 586/ 753 844 995
No comments:
Post a Comment