Monday, January 05, 2015

WANACCM WASHAURIULIWA KUTOMBEZA PROFESA TIBAIJUKA

Wanachama na wapenzi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wametakiwa   kudumisha umoja na mshikamano  miongoni mwao badala kuendekeza tabia ya inayokigharimu chama hicho kwa sasa  inayofanywa na baadhi  wanachama wa chama hicho ya kutafunana wenyewe  kwa wenyewe.

Wito huo umetolewa  leo na IDD ALI AME ambaye katibu  wa CCM mkoani Kagera wakati wa kikao cha kutathimini  na kujadili masuala ya maendeleo katika wilaya ya MULEBA kilichoandaliwa na PROFESA ANNA TIBAIJUKA, mjumbe wa halmashauri  kuu ya CCM taifa (NEC) na mbunge jimbo la MULEBA KUSINI kilichofanyika kwenye jengo la taasisi ya KAJUMULO  ambacho kiliwashirikisha viongozi wa chama hicho kuanzia ngazi ya mashina  hadi wilaya.

AME amesema  ikiwa wanachama wa CCM wataendekeza tabia ya  kutafunana wenyewe kwa wenyewe wataleta mpasuko ndani ya chama hali itakayovipa nafasi vyama vya upinzani  ya kushinda chaguzi mbalimbali  jambo litakalochangia kukichimbia  chama hicho kaburi.


Kwa upande wao , DEOGRATIAS RUTAGUMWA, katibu wa CCM wa mkoa wa KILIMANJARO  na DIDAS ZIMBIILE , katibu wa jumuia ya umoja wa vijana mkoani KAGERA  wanawashauri wananchi wilayani MULEBA  kuzipuuza kauli zinazotolewa na wapinzani,   Naye PROFESA ANNA TIBAIJUKA anaeleza mikakati yake na namna masuala ya kuendeleza elimu yalivyomgharimu, huku ERNESTINA RICHARD, katibu wa wazazi wa mkoa wa KAGERA anawaomba wananchi wawe na imani na PROFESA TIBAIJUKA.


Profesa Tibaijuka  amewaahidi wananchi kuwa ataendelea kutetea nafasi yake ya ubunge pamoja na kuwajibishwa na kufuatia tuhuma za fedha alizozipata toka kwa RUGEMALILA.

No comments:

Post a Comment