Thursday, October 18, 2012

MPANGO WA JESHI LA POLISI LA KUWAPIMA WANANCHI KWA HIARI WACHANGAMKIWA





Mganga mkuu wa jeshi la polisi mkoani Kagera Dr. Husein Gamu, ambaye amehamasisha mpango mzima  wa kuwapima vipimo vya UKIMWI kwa  hiari  zoezi hilo lilifanyika eneo la standi kuu ya mabasi iliyoko katika manispaa ya Bukoba na kuhudhuriwa na watu wengi hususani vijana.

Wednesday, October 17, 2012

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI ATEMBELEA BANDARI A BUKOBA NA KEMONDO

Naibu waziri wa uchukuzi Charles Tizeba akitoa maelekezo kwa maofisa wa bandari alipotembelea bandari ya Bukoba.
Meli ya mizigo ikipakia sukari ilikutwa bandari ya Bukoba.
 Tibeza akiongea na wasafiri aliowakuta bandarini.
 Baadhi ya wasafiri ambao walikutwa kwenye jumba la wageni lililoko bandaria ya Bukoba.
 Naibu waziri akiangalia huduma zinazotolewa na meli ya Victoria.
Sehemu ya mandhari ya bandari ya Bukoba.
 Naibu waziri akielezwa huduma zinazotolewa na kampuni inayomiliki meli ya Victoria.
Meli kongwe nchini ya victoria ambayo hufanya safari zake kati ya mikoa ya Mwanza na Bukoba, ilikuwa imeegeshwa bandari ya Bukoba, Naibu waziri ameutaka uongozi wa kampuni ya meli kuhakikisha unaweka mazingira mazuri kwa wasafiri ambayo ni pamoja na kuiwekea meli hiyo viyoyozi ili wasafiri waweze kuvuta hewa nzuri na pia waifanyie usafi kwenye maeneo yote.

PINDA JIJINI LONDON

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  na mkewe Tunu wakiwa  na Mtangazaji wa Shirika la Habari la Uingereza BBC, Zawadi Machibya (kulia) wakati alipozungumza na Watanzania waishio Uingereza, kwenye Ubalozi wa Tanzania uliopo London Oktoba 16, 2012. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI MKOANI KAGERA

 Mkuu wa mkoa wa Kagera Kanali mstaafu Fabian Massawe akitoa taarifa kwa naibu waziri wa uchukuzi Charles Tibeza aliyefanya ziara ya siku moja mkoani Kagera.
Baadhi ya viongozi wa serikali na mamlaka ya bandari nchini wakimsikiliza Naibu waziri Tibeza.
Naibu waziri wa uchukuzi akijibu hoja za taarifa iliyotolewa na Massawe mkuu wa mkoa wa Kagera.
 Massawe (Kulia) kimsikiliza kwa makini Naibu waziri Tibeza anayefuata ni mjumbe wa sekretarieti ya mkoa wa Kagera Seif Husein na kushoto ni mjumbe mwingine Fikir Kisimba.
 Mhandisi wa kampuni ya ukandarasi ya CGG- MECCO JV inayojenga uwanja wa ndege wa Bukoba, Patric Kain akitoa sababu zinazokwamisha ujenzi wa uwanja wa Ndege, mhandisi huyo alishindwa kumpa taarifa sahihi Naibu waziri Tibeza.
 Naibu waziri Tibeza akitoa maelekezo kwa kampuni inayofanya ya ujenzi wa uwanja wa Bukoba, waziri huyo alionyeshwa kutoridhishwa na taarifa kasi ya ujenzi wa uwanja huo.
 Baadhi ya viongozi wakimsikiliza Naibu waziri Tibeza alipoyembelea uwanja wa ndege wa Bukoba.
 Sehemu ya uwanja wa ndege wa Bukoba unaofanyiwa ukarabati.
Massawe akijadiliana jambo na Naibu waziri Tibeza na watendaji wengine walienda kuona hali ya ujenzi wa uwanja wa ndege wa Bukoba.

Tuesday, October 16, 2012

CHIZZA AONYESHA MAKEKE YAKE MKOANI KAGERA

WAZIRI wa ushirika, chakula na masoko Mhandisi Christopher Chizza amewahimiza viongozi na wanachama wa vyama vya ushirika nchini kushikamana  ili waweze kuendeleza  na kuviimarisha vyama vya vyao badala ya kujenga dhana ya kuvididimiza.    

Mhandisi Chizza aliyasema hayo jana wakati wa kikao chake na viongozi wa serikali ya mkoa wa Kagera, uongozi wa chama cha ushirika Kagera (KCU) na waandishi wa habari kilichofanyika kwenye ukumbi wa mkuu wa mkoa wa Kagera.

Katika kikao hicho alisema migongano  zinazojitokeza kati ya  baadhi  ya wanachama wanaounda vyama ushirika na waliopewa jukumu la kusimamia na kuongoza vyama vya ushirika kamwe haziwezi kuviimarisha na kuviendeleza vyama vya ushirika.

Alisema kuwa duniani kote migongano ndio huwa chanzo cha kudidimiza vyama vya ushirika, Chizza alisema ili vyama vya ushirika viweze kuimarika na kuendelea  ni lazima wana ushirika wapendane, waaminiane na waheshimiane, “hizi  ndio nguzo kuu zinazoimarisha ushirika”alisema kwa msisitizo.

“Ndugu zangu viongozi wa KCU ninapokea barua rundo zinazowatuhumu, nyingine zinazoelea masuala ya ubadhilifu na barua hizi zinaandikwa na wanaushirika wenu, ila taarifa mliyonipa ya utendaji wa kazi naiona iko wazi na inaelezea hali halisi ya utendaji kazi mzuri wa KCU, sasa sielewi hizi barua zinaashiria kitu gani” alisema kwa msangao.

Aliuagiza uongozi wa KCU kuwawajibisha watendaji ndani ya ushirika huo wanawaona wanajihusisha na masuala ya ubadhilifu wa mali ya wakulima, alisema yoyote wanayemuona anajihusisha na masuala ya ubadilifu wasiishie kumfukuza tu bali wamfikishe mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa KCU, John Binunshu katika taarifa yake kwa waziri huyo aliiomba serikali isitoe vibali  vya kununua kahawa moja kwa moja toka kwa wakulima kwa  makampuni makubwa ambayo ununua kahawa inayakusanywa na vyama vya ushirika moja kwa moja mnadani.

Binunshu alisema kuwa hali ya serikali kutoa vibali kwa makampuni hayo makubwa inadhoofisha vyama vya ushirika kwa kuwa yanachangia mnada wa kahawa kuchelewa, alisema minada ya kahawa inapochelewa vyama vya ushirika vinakosa fedha za kuwalipa wakulima hivyo vinalazimika kununua kahawa kwa mkopo.

Akitoa ufafanuzi juu ya kwa nini baadhi ya wanunuzi wa kahawa wananunua kahawa kwa bei kubwa alisema, wanaonunua kahawa kwa bei kubwa ni wale wanaonunua kahawa bila kutumia minzani, aliendelea kuwa wanunuzi hao wananunua kahawa kwa ujazo badala ya kilo jambo ambalo linawapunja wakulima.

Mkuu wa wilaya ya Bukoba Bi. Ziporah Pangani alikiri kuwepo kwa magendo ya kahawa, alisema kamati yake ya ulinzi na usalama inalishughulikia suala hilo, alimaliza kwa kusema kuwa kamati yake imeshakamata magari yaliyokuwa yanavusha kahawa kwa njia ya magendo na kufilisi kahawa hiyo.

MKUU WA MKOA KAGERA AMUUMBUA MBUNGE WA JIMBO LA NKENGE

Huyu ndiye mbunge wa jimbo la Nkenge Asumpta Mshama.

MKUU wa mkoa wa Kagera Kanali Mstaafu Fabian Massawe amepinga vikali ushauri  uliotolewa mbunge wa jimbo la Nkenge Asumpta Mshama  wa kuiomba serikali iwaruhusu wakulima wao wenyewe wajitafitie masoko wa kahawa wanayoizalisha ndani na nje ya nchi.

Massawe amesema kamwe biashara ya kahawa haitakuwa huria hivyo wakulima wataendelea na utaratibu uliowekwa na serikali wa kuuza kahawa yao kwenye vyama vya ushirika na makampuni ya yaliyosajiliwa kisheria yanayofanya kazi ya kununua kahawa toka kwao.

Mkuu huyo wa mkoa alitoa kauli hiyo wakati wa kikao cha kamati ya ushauri ya mkoa wa Kagera kilichofanyika jana kwenye ukumbi wa mkuu wa mkoa uliko kwenye manispaa ya Bukoba.

Alisema kuwa wakulima wanapouza kahawa kwa njia isiyo rasmi wanakuwa wanaikosesha serikali mapato , “halmashauri za wilaya na manispaa huwa zinanufaika na mauzo ya kahawa kwa kupata ushuru tukiruhusu biashara huria ya kahawa tutakuwa tuaziua halmashauri za wilaya na manispaa” alisema Massawe.

“Sikubaliani na kauli ya mhemimiwa mbunge biashara ya kahawa kamwe haitakuwa huria, na mimi naahidi titaendelea kuwashughulikia kikamilifu wale wote wanajihusisha biashara ya magendo ya kahawa, ni lazima tuunusuru uchumi wetu” alisema huku akishangiliwa.

Massawe alisema kamwe hatamfumbia macho mtu yoyote atakayejihusha na magendo ya kahawa’ “Nitamshughulikia mtu yoyote bila kuangalia sura yake, kabila na nafasi yake aliyonayo ndani ya jamii” alisema.

Aliwataka viongozi wote washirikiane ili wawezer kuwathibiti wale wote wanajihusisha na magendo ya kahawa, alisema magendo ya kahawa inavidhoofisha vyama vya ushirika na wakulima wanaouza kahawa yao kwa njia ya magendo, “wakulima wanaouza kahawa kwa njia ya magendo wanapunjwa sana” alimaliza kusema.