Tuesday, February 10, 2015

TOENI MAONI JUU YA SAKATA LA FEDHA ZA AKAUNTI YA ESCROW

Ndugu watembelea mtandao wangu kuna suala ambalo limeibuka linalohusiana na sakata la Fedha alizolipwa Father Rugemalila toka Account ya ESCROW, wengi wametoa tafsiri mbalimbali juu ya fedha ambayo ni mali halali ya Bw. Rugemalila, naomba tupeane ushauri hivi ni haki kuwawajibisha wale walipewa mgao wa fedha hiyo kama zawadi toka kwa RUGEMALILA? au mnaonaje sakata hilo lina mlengo wa masuala ya kisiasa hasa tunapoelekea kwenye uchaguzi mkuu 2015? kazi kwenu ndugu watembeleaji wa mtandao www.audax-kagera.blogspot.com.

Na mhariri

MKOA WA KAGERA WAJIZATITI KUTHIBITI VIFO VYA WAKINA MAMA WAJAWAZITO NA WATOTO

www.bukobawadau.blogspot.comwww.issamichuzi.blogspot.com


NA AUDAX MUTIGANZI

BUKOBA


Kamati ya huduma ya afya ya msingi  katika mkoa wa KAGERA imefanya kikao cha dharura kwa lengo la kujadili na kuweka mikakati mbalimbali yenye lengo la kupunguza  vifo vya watoto wachanga chini ya umri wa miaka MITANO na wakina mama wajawazito.


Kikao hicho kimefanyika wilayani KARAGWE  kwenye ukumbi wa  hoteli ya kanisa la kiinjili la KIRUTHERI  diosisi ya KARAGWE iliyoko katika mji wa mdogo  wa KAYANGA chini ya mkuu wa mkoa wa  KAGERA, JOHN MONGELLA.


Katika kikao hicho kilichohudhuliwa na  viongozi mbalimbali wa serikali katika ngazi zote, mkuu huyo wa mkoa amewaagiza wakuu wa wilaya mkoa humo  katika kila vikao wanavyoviandaa  vya kujadili masuala mbalimbali ya maendeleo kuweka ajenda ya namna ya kudhibiti vya vifo vya watoto wachanga chini ya miaka MITANO na  wakina mama wajawazito.





DKT THOMAS RUTACHUNZIBWA ni mganga mkuu wa mkoa wa KAGERA na NEEMA KYAMBA mratibu wa huduma ya watoto na wakina mama wajawazito  katika mkoa huo ni maofisa wa afya wanaoeleza  hali ya sasa ya  vifo vya watoto na wakina mama.




 Kwa upande wake GRANDIOSA TIBAIJUKA  ambaye ni meneja taaluma wa mradi wa JHPIEGO unaofadhiliwa na seriikali ya MAREKANI  anaishauri jamii kuchangia huduma ya afya ili iweze kupata matibabu sahihi badala ya kutegemea sana misaada toka kwa serikalini  na wafadhili, DALI  RWEGASIRA mkuu wa wilaya ya KARAGWE na DENIS MBEO mkuu wa wa wilaya ya BIHARAMULO ni miongoni mwa wakuu wa wilaya wanaoeleza mikakati yao ya  namna ya kuthibiti vifo vya wakina mama na watoto kwa kuwahamasisha  wananchi wajiunge na mfuko wa afya ya jamii.




Mkoa wa Kagera ni miongoni mwa mikoa michache hapa nchini ambazo inafanya mikakati mikubwa ya kuhakikisha vifo vya wakina mama wajawazito na watoto cinini ya miaka MITANO vinabaki kwenye vitabu vya historia, mkakati wa mkoa huo ni kuihamasisha jamii namna ya kujiepusha na vifo hivyo kuanzia ngazi ya vijiji, mtaa na vitongoji.

WAZIRI MKUU ATEMBELEA SHAMBA LAKE

 waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwaongoza viongozi wa Kanisa la Anglican kutembelea malisho ya ng'ombe  kwenye shamba lake  lililopo  Zuzu Dodoma Februari 9, 2015. Baadhi ya viongozi hao ambao walikwenda kujifunza kwa lengo la kuanzisha shamba linalofanana na hilo Dodoma ni Askofu Dickson Chilongani wa Dayosisi ya Dodoma (wapili kushoto), Askofu Maimbo Mndolwa wa Dayosisi ya Tanga (kulia kwake) na kulia ni Re. Canon, Johnson Chinyongole ambaye ni Katibu Mkuu wa Kanisa hilo. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


DR KAMALA ATEMBELEA MAONYESHO YA UTALII BRUSELS

 Balozi wa Tanzania Ubeligiji Dr. Diodorus Buberwa Kamala akimshukuru mwakilishi wa kampuni ya utalii ya Escape Bwana Nassri Chaouki baada ya kutembelea banda la kampuni hiyo inayoshiriki Maonesho ya Utalii ya Brussels. Balozi Kamala aliishukuru kampuni hiyo kwa kutangaza vivutio vya utalii vya Tanzania.

 Balozi wa Tanzania Ubeligiji Dr. Diodorus Buberwa Kamala P AKIWA katika picha ya pamoja na Bwana Burt Munting Mkurugenzi wa kampuni ya utalii ya Habari Travel ya Uganda inayoshiriki Maonesho ya Utalii ya Brussels. Balozi Kamala ameishukuru kampuni hiyo kwa kutangaza vivutio vya utalii vinavyopatikana Tanzania.
Balozi wa Tanzania Ubeligiji Dr. Diodorus Buberwa Kamala P akiwa katika picha ya pamoja na Meneja wa Masoko wa kampuni ya kutangaza utalii ya Travel Xenarjo ya Ubeligiji Bi. Dana Maes baada ya kutembelea Banda la kampuni hiyo inayoshiriki Maonesho ya Utalii ya Brussels. Kampuni hiyo imekubali kutangaza vivutio vya utalii vinavyopatikana Tanzania baada ya Balozi Kamala kuiomba kampuni hiyo kufanya hivyo.

KIKAO CHA HALMASHAURI KUU YA WILAYA YA BUKOBA VIJIJINI


Monday, February 09, 2015

WAZIRI MKUU AZINDUA MPANGO WA KUKUZA STADI ZA KKK *Ataka AZISE zishirikishwe kikamilifu



WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amezindua Mpango wa Kitaifa wa Kukuza Stadi za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK) unaolenga kukuza viwango vya uelewa kwa watoto wa darasa la kwanza na la pili kwa nchi nzima.

Mpango huo wa miaka mitatu ulioanza kutekelezwa 2014/2015 hadi 2016/2017 umelengwa kuwahusisha watoto wenye umri wa miaka mitano hadi 13 walio kwenye mfumo rasmi wa elimu na usio rasmi (MEMKWA).

Akizungumza na wadau wa elimu, walimu na wanafunzi walioshiriki uzinduzi huo jana jioni (Jumamosi, Februari 7, 2015) Waziri Mkuu Pinda alisema mpango huo ni mkubwa na umeandaliwa mahsusi kujibu changamoto zilizojitokeza miaka ya nyuma.

Aliwataka watekelezaji wakuu wa mpango ambao ni Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) pamoja na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kuhakikisha kuwa wanazishirikisha asasi zisizo za Kiserikali ambazo zinajihusisha na masuala ya elimu.

“Kuna mashirika mengi yasiyo za kiserikali ambayo ni chachu ya kuhimiza elimu nchini... jaribuni kuwashirikisha sababu wao ni wadau wazuri sana wa suala hili. Pangeni utaratibu wa kukaa na hawa wadau na kuwapa mrejesho wa mpango huu mzima,” alisema Waziri Mkuu.

Hata hivyo, Waziri Mkuu aliwataka wahusika wakuu wa mpango waangalie mgawanyo wa mikoa iliyoingizwa kwenye mpango huo kwa kuzingatia kanda ili kuleta matokeo ya mtawanyiko badala ya hali ilivyo sasa. “Nimeangalia jinsi mlivyogawa mikoa yenu, inanipa taabu kidogo... kuna mikoa inahitaji msukumo wa pekee, mikoa ya wadugaji, mikoa iliyoko pwani ya bahari na maziwa, yote inahitaji msukumo wa tofauti,” alisema.

Katika taarifa yao, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ilisema mpango huo wa KKK au LANES (Literacy and Numeracy Support Programme)  unafadhiliwa na Ushirika wa Kimataifa wa Maendeleo ya Elimu (Global Partnership for Education – GPE) na wahisani wengine.


Wahisani hao ni pamoja na Shirika la Maendeleo la Uingereza (DFID) kupitia mradi wa EQUIP-T unaotekelezwa katika mikoa saba ya Kigoma, Shinyanga, Mara, Simiyu, Lindi, Dodoma na Tabora; Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Elimu kwa Mtoto (UNICEF) wanaofadhili utelekezaji wa Mpango wa LANES katika mikoa ya Iringa, Mbeya na Njombe; na Shirika la Maendeleo la Marekani (USAID) kupitia Mradi wa TZ-21 unaotekelezwa katika mkoa wa Mtwara.

Mapema, akisoma taarifa ya mpango huo mbele ya Waziri Mkuu, Kamishna wa Elimu nchini, Prof. Eustella Bhalalusesa alisema mpango huo umelenga kuongeza ufanisi katika stadi za KKK, kurahisisha kazi ya walimu wanaofundisha watoto wa darasa la kwanza na la pili pamoja na kuongeza ushiriki wa jamii katika kuboresha elimu na hasa ujifunzaji wa stadi za KKK.

Alisema mpango huo utachangiwa sh. bilioni 150 ambazo zitaingizwa moja kwa moja kwenye mfuko wa elimu kupitia Wizara ya Fedha.

Alisema maandalizi yote ya utekelezaji wa mpango huu yamekamilika ikiwa ni pamoja na mtaala wa darasa la kwanza na darasa la pili, muhtasari wa KKK kwa darasa la I & II, pamoja na Mwongozo wa Mwalimu wa kufundisha kusoma kuandika na kuhesabu.

(mwisho)


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
S. L. P. 980,
DODOMA.
JUMAPILI, FEBRUARI 8, 2015.