Tuesday, March 31, 2015

JESHI LA POLISI KAGERA LAWANASA WATU WAWILI WALIKUWA WAKIUZA VIUNGO VYA ALBINO

Watuhumiwa waliokuwa wakiuza viungo walipata viungo hivyo ambavyo ni pamoja na mifupa na mafuvu kwa kuchimba kaburi la Laston Bartazar John  mkazi aliyekuwa mkazi wa kijiji cha Kandegesho kilichoko wilayani Karagwe, walikuwa wakiuza viungo hivyo kwa shilingi milioni 20, watuhumiwa hao walikamatwa eneo la kyaka kwenye hoteli ya FORD chumba namba 1, walikuwa kwenye harakati za kusafirisha viungo hivyo Maeneo ya Runzewe kwa lengo la kuviuza.



Mabaki ya mifupa waliyokutwa nayo watuhumiwa.
Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Kagera, Henry Mwaibambe akionyesha baadhi ya viungo.
Kamanda akiwaonyesha watuhumiwa.



Hili ni fuvu.

Meno hayo.

Sunday, March 29, 2015

MATUKIO YA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiteta na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo  ya Makazi, Angela Kairuki, Bungeni mjini Dodoma.
Waziri wa Fedha Saada Mkuya  akihitimisha Muswada  wa Sheria ya Bajeti wa Mwaka 2014, Bungeni mjini Dodoma.

SHEREHE YA KUMUAGA MKUU WA MKOA WA ZAMANI WA KAGERA KANALI MSTAAFU FABIAN MASSAWE NA KUMKARIBISHA MKUU WA MKOA WA SASA JOHN MONGELLA

 Mkuu wa mkoa wa Kagera, John Mongelaa akishiriki kuimba wimbo wa hamasa katika mkoa wa Kagera ulioasisiwa na Kanali Massawe.
 Baadhi ya wakuu wa wilaya katika mkoa wa Kagera walioudhuria sherehe hiyo.
 Wakuu wa wilaya.
 Baadhi ya viongozi wa madhehebu ya dini, katika ni askofu msaidizi wa jimbo la Bukoba Methodius Kilaini.
 Mama Massawe (kulia) na Mama Mongella (kushoto).



 Baadhi ya wajumbe wa kamatiya ulinzi na usalama ya mkoa wa Kagera, kulia ni kamanda wa jeshi la polisi Kagera, Henry Mwaibambe, George Kombe afisa wa idara ya uhamiaji mkoa wa Kagera na mkuu wa TAKUKURU , Mwaiselo.
 Mambo ya keki hayo.

 Mkuu wa wilaya ya Karagwe, Dali Rwegasira akifaya vitu vyake.
 Kanali mstaafu Massawe akiwaaga wananchi wa mkoa wa Kagera, amewasisitiza wananchi kuchangamkia fursa za umoja wa nchi za afrika mashariki, pia amewataka wananchi kujiepusha na vitendo vinavyohatarisha amani, na mambo yanayochangia umaskini.


 Baadhi ya waandishi wa habari walioudhuria sherehe hiyo, kutoka kushoto, Charles Mwebeya (TBC), Audax Mutiganzi wa CLOUDS TV na mmiliki wa mtadao huu wa kijamii na Mariam Emily wa STAR TV.
Hawa pia ni waandishi wa habari walioudhuria sherehe hiyo, nyuma kulia ni Alen Sylivery wa ITV na Sylvester Raphael afisa habari wa ofisi ya mkuu wa mkoa Kagera.

Thursday, March 26, 2015

Rais Kagame ahudhuria mkutano wa Wakuu wa Nchi za Kanda ya Kati jijini Dar es salaam

  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimraribisha Rais Paul Kagame wa Rwanda kwenye ukumbi wa Mikutano wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Kanda ya Kati (Central Corridor Conference) ulioanza jana na kumalizika leo Machi 26, 2015
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete na wageni wake Rais Paul Kagame wa Rwanda na Rais Pierre Nkurunzinza kwenye ukumbi wa Mikutano wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Kanda ya Kati (Central Corridor Conference) ulioanza jana na kumalizika leo Machi 26, 2015.

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete na  Rais Paul Kagame wa Rwanda wakisiliza maelezo toka kwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania Bw. Rished Bade walipotembelea kituo cha kulipia ushuru wa aina zote chini ya paa moja  katika bandari ya Dar es salaam leo Machi 26, 2015.

Rais Paul Kagame wa Rwanda akipeperusha bendera kuashiria kuzinduliwa kwa safari za treni za mizigo kuelekea Rwanda katika stesheni ya reli ya Dar es salaam akiwa na mwenyeji wake Rais Jakaya Mrisho kikwete leo Machi 26, 2015

UZINDUZI WA BODI YA PAROLE YA MKOA WA KAGERA

 Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Kagera Henry Mwaibambe  na mkuu wa gereza la Bukoba walikuwa miongoni mwa walioudhuria uzinduzi huo.

 Mkuu wa mkoa wa Kagera, John Mongella akizungumza na walioudhuria uzinduzi wa bodi ya Parole ya mkoa wa Kagera.
 Baadhi ya maofisa wa jeshi la magereza kagera.
 Mkuu wa jeshi la magereza mkoani Kagera, Omary Mtinga (kulia) akitafakari jambo wakati wa uzinduzi huo.
 Askofu msaidizi wa jimbo la Bukoba, Methodius Kilaini (kushoto) ni mwenyekiti wa bodi ya Parole ya mkoa wa Kagera.