Thursday, February 26, 2015

PATO LA MWANANCHI MBEYA LAVUKA LENGO LA KITAIFA

     
                                                 
 WAZIRI MKUU Mizengo Pinda ameupongeza uongozi wa mkoa wa Mbeya kwa kuvuka lengo la wastani wa pato la mwananchi kitaifa na kuwataka waendeleze kasi ya kupambana na umaskini kwa wakazi wa mkoa huo.

Ametoa pongezi hizo jana usiku (Jumanne, Februari 24, 2015) wakati akizungumza na viongozi wa mkoa huo na wilaya zote wakiwemo wadau mbalimbali na viongozi wa dini mara baada ya kupokea taarifa ya Mkoa wa Mbeya.

Alisema katika mipango yake, Serikali ililenga kwamba pato la mtu kwa mwaka liwe sh. 1,186, 200, lakini kwa sababu ya jitihada mbalimbali mkoa huo umelivuka. “Katika taarifa aliyonisomea, Kaimu Mkuu wa Mkoa amesema wastani wa pato la mwananchi umeongezeka kutoka sh. 711,201/- mwaka 2008 hadi kufikia sh 1,420,427/- mwaka 2013 na kwamba mkoa unachangia asilimia 7.43 ya Pato la Taifa,” alisema.

Alisema kipato cha mtu mmoja kwa siku ni sh. 3,891/- ambazo ni zaidi ya Dola mbili za Marekani (sh. 3,400/-). “Wakubwa hawa wanatupima kwa kuangalia kipato cha mtu kwa siku. Wanasema nchi ni maskini iwapo watu wake wanaishi chini ya dola moja kwa siku (sawa na sh. 1,700/-).”

“Mbeya imeendelea kushika nafasi ya tatu kwa kuchangia vizuri Pato la Taifa ikiwa imetanguliwa na Dar es Salaam na Iringa. Ninawapongeza kwa sababu mmevuka malengo ya Taifa katika eneo la pato la mtu mmoja mmoja,” alisema Waziri Mkuu.

Mapema, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Bw. Deodatus Kinawilo ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Chunya, alisema pato la mkoa limeongezeka kutoka sh. trilioni 1.779 mwaka 2008 na kufikia sh. trilioni 3.951 mwaka 2013. 

“Uchumi wa mkoa huu unategemea kilimo, ufugaji, uchimbaji madini, uvunaji mazao ya maliasili, biashara, uzalishaji viwandani na ajira katika taasisi za serikali na sekta binafsi,” alisema.

Wakati huohuo, uongozi wa mkoa wa Mbeya umetakiwa kuongeza bidii ili uweze kuinua kiwango cha ufaulu wa elimu ya kwa sababu umekuwa ukiendelea kushuka na kuwa chini ya kiwango cha asilimia 60 kilichowekwa na Serikali.

Waziri Mkuu aliutaka uongozi huo ubuni mbinu za kisomi zitakazowawezesha wanafunzi wa shule za msingi kuelewa wanachofundishwa, hivyo, kufaulu mitihani yao vizuri. ”Ufaulu wenu kwa shule za msingi ni asilimia 46.6, uko chini ya kiwango cha kitaifa cha ufaulu kwa asilimia 13.4. Ni matokeo yasiyoridhisha, fanyeni utaratibu maalum ili yapande,” alisema.

(mwisho)

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATANO, FEBRUARI 25, 2015.


Wednesday, February 25, 2015

MKUU MPYA WA WILAYA YA MISENYI AAPISHWA

 Mkuu wa wilaya ya Bukoba, Jaskon Msome kulia kabla alikuwa mkuu wa wilaya ya Musoma.
 Mkuu mpya wa wilaya ya Misenyi, Fadhil Nkurlu kulia, kabla ya kuapishwa.
 Baadhi ya viongozi wa dini walioudhuria sherehe ya kuapishwa kwa mkuu mpya wa wilaya ya Misenyi.

 Baadhi ya wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa wa Kagera.







Tuesday, February 24, 2015

RAIS KIKWETE AMKABIDHI H.H. THE AGA KHAN HATI YA CHUO KIKUU CHA AGA KHAN KILICHOPO DSM



  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Kiongozi wa madhehebu ya
Ismailia duniani Mtukufu Aga Khana hati ya Chuo Kikuu cha Aga Khan
kilichopo Dar es salaam leo February 23, 2015 Ikulu jijini Dar es
salaam
.
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimsikiliza  Kiongozi wa madhehebu ya
Ismailia duniani Mtukufu Aga Khana akiongea baada ya kumkabidhi hati
ya Chuo Kikuu cha Aga Khan kilichopo Dar es salaam leo February 23,
2015 Ikulu jijini Dar es salaam
.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Kiongozi wa madhehebu ya
Ismailia duniani Mtukufu Aga Khana baada ya kumkabidhi hati ya Chuo
Kikuu cha Aga Khan kilichopo Dar es salaam leo February 23, 2015 Ikulu
jijini Dar es salaam
.

Saturday, February 21, 2015

RAIS KIKWETE AWA MWENYEKITI MPYA WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI

 Rais Jakaya Kikwete,Naibu Rais wa Kenya,William Rutto na maafisa
wengine wakiwa kwenye Jengo la mikutano wa kimataifa la Kenyatta
International Convention Center(KICC)Nairobi,Kenya wakati wa kuimba
wimbo wa taifa la Tanzania katika mkutano wa kawaida wa 16 wa Wakuu wa
nchi za Afrika Mashariki.

Kutoka kushoto ni mgeni mwalikwa,Rais wa Sudani Kusini,Salva Kiir,Rais
wa Burundi,Pierre Nkurunziza,Rais Jakaya Kikwete(Tanzania),Rais Uhuru
Kenyatta(Kenya)Rais Yoweri Museveni(Uganda)Rais Paul Kagame(Rwanda)na
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki(EAC)Dk Richard Sezibera
wakiwa kwenye ukumbi wa mikutano kwenye  mkutano wa kawaida wa 16 wa
Wakuu wa nchi za Afrika Mashariki.

Rais Jakaya Kikwete(kushoto)akipokea bendera ya Afrika
Mashariki(EAC)kutoka kwa Rais wa Kenya,Uhuru Kenyatta ikiwa ni ishara
ya kumkabidhi Uenyekiti wa  EAC  kwenye  mkutano wa kawaida wa 16 wa
Wakuu wa nchi za Afrika Mashariki uliofanyika leo.20/2/2015

PICHA NA IKULU

SERIKALI KUAJIRI WALIMU 35,000 - WAZIRI MKUU



WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amesema Serikali imepanga kuajiri walimu
zaidi ya 35,000 kwa ajili ya shule za sekondari ili kukabiliana na
tatizo la uhaba wa walimu nchini.

Ametoa kauli hiyo jana jioni (Alhamisi, Februari 19, 2015) wakati
akizungumza na mamia ya wakazi wa kata ya Kiwere, mara baada ya
kukagua ujenzi wa maabara na kuzindua nyumba nne za walimu kwenye
shule ya sekondari ya Kiwere, tarafa ya Kalenga, wilayani Iringa.

Waziri Mkuu alisema walimu hao watagawanywa kwenye shule kulingana na
mahitaji yaliyokwishawasilishwa na kwamba watakapopata mgao wao hawana
budi kuziangalia kwanza shule zenye miundombinu iliyokamilika kama
ilivyo kwa shule hiyo.

Akifafanua kuhusu kasi ya ujenzi wa maabara Waziri Mkuu alisema: “Mkoa
mzima wa Iringa unahitaji kuwa na maabara 318 na zilizo tayari mpaka
sasa ni 108. Lakini kuna nyingine 141 ambazo zimekwishaanza kujengwa
na zimefikia hatua nzuri. Nimeambiwa katika muda mfupi ujao kutakuwa
na maabara 249 zilizokamilika,” alisema.

“RC inabidi uwasukume watu wako ili hizi 69 ambazo bado hazijaanza
kujengwa zikamilike kabla ya Juni mwaka huu kama ambavyo Mheshimiwa
Rais Jakaya Kikwete alikuwa ameelekeza. Alisema hataongeza tena muda
wa ujenzi,” aliongeza.

Alisema elimu ni sekta ya msingi ambayo Serikali imeamua kuipa umuhimu
wa kipekee na kuiweka katika moja ya maeneo sita muhimu ya kipaumbele
chini ya Mpango wa Matokeo Makubwa ya Haraka (BRN).

Waziri Mkuu aliwataka wanafunzi wa shule hiyo wasome kwa bidii na wawe
wasikivu ili waweze kufanya vizuri zaidi kwenye masomo yao.

Mapema, akitoa taarifa mbele ya Waziri Mkuu, Afisa Elimu wa Wilaya ya
Iringa, Bw. Leonard Msigwa alisema ujenzi wa nyumba hizo nne ambazo
zina pande mbili (four duplex houses) umegharimu sh. milioni 323.2.
Alisema nyumba hizo zenye vyumba vitatu vya kulala, sebule na jiko,
zina uwezo wa kubeba familia nane.

Bw. Msigwa alisema ujenzi wa nyumba ulifanywa shirika la DESWOS la
Ujerumani kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Iringa pamoja
na wananchi. Pia walisaidiwa kujengewa tenki la maji na mabweni mawili
yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 112 kila moja kwa ajili ya
wasichana.

Akifafanua kuhusu hali ya ujenzi wa maabara, Afisa Elimu huyo alisema
hadi sasa wamekamilisha ujenzi wa vyumba viwili vya Kemia na Baiolojia
lakini bado viko kwenye hatua ya kupaka rangi. Alisema mfumo wa gesi
na maji umekwishafungwa ndani ya vyumba vya maabara.

“Ujenzi wa maabara hadi sasa umekwishagharimu sh. milioni 52.8/- na
katika kipindi cha Februari 2015, tumefanikiwa kutengeneza baadhi ya
samani za maabara yaani meza 24 na stuli 96 zenye thamani ya sh.
8,940,000/-,” alisema.

WAZIRI MKUU ATAKA WATANZANIA WAWE NA HOFU YA MUNGU




WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amewataka Watanzania wasikilize na kufuata
mafundisho yanayotolewa na viongozi wa dini ili Tanzania iwe nchi
yenye watu waadilifu na wenye hofu ya Mungu.

Ametoa wito huo leo mchana (Ijumaa, Februari 20, 2015) wakati
akizungumza na maelfu ya waumini na wananchi waliohudhuria ibada ya
mazishi ya Askofu Mstaafu Magnus Mwalunyungu kwenye kanisa la Moyo
Mtakatifu wa Yesu la Tosamaganga, Jimbo Katoliki la Iringa.

“Leo ni siku ya pekee ya kuwasikiliza viongozi wa dini wakituasa
tujiandae kwa maisha baada ya kifo. Tukio hili la leo litupe nguvu ya
kukubali kwamba kifo kipo licha ya kuwa hakizoeleki na kinapotokea
kinaleta simanzi kubwa,” alisema.

“Ninawasihi Watanzania wote tufuate mafundisho yanayotolewa na
viongozi wa dini zetu ili Tanzania iwe na kundi la watu wenye hofu ya
Mungu, waadilifu na wanyofu kama ambavyo mahubiri ya leo
yamesisisitiza,” alisema.

Waziri Mkuu ambaye yuko kwenye ziara ya siku tano ya kikazi mkoani
Iringa, aliamua kusitisha ziara yake siku ya leo ili aweze kushiriki
msiba huo. Pia alitoa salamu za rambirambi kwa niaba ya Rais Jakaya
Kikwete ambaye yuko Kenya kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya
ya Afrika Mashariki.

Akitoa mahubiri kwenye ibada hiyo, Askofu Damian Dallu wa Jimbo Kuu
Katoliki la Songea alisema wanadamu wanahangaika na kuogopa kifo kwa
sababu hawajui baada ya kifo maisha yao yatakuwaje.

“Askofu Mwalunyungu ameishi kwa miaka 85 na kati ya hiyo, miaka 55
alikuwa akitumikia kama padre na kwa miaka 22 alimtumikia Mungu aakiwa
Askofu. Na hata baada ya kustaafu aliomba awe Parokopale Kidamalai
ambako alitumikia kwa miaka minne. Maisha yake yanaendana na neno
kutoka kitabu cha hekima kwamba kifo cha mwadilifu ni kupumzika kwa
starehe,” alisema.

Ibada hiyo ya mazishi ilihudhuriwa na Maaskofu wa kanisa katoliki zaidi ya 20.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
IJUMAA, FEBRUARI 20, 2015.

Thursday, February 19, 2015

KIKAO CHA KAWAIDA CHA BARAZA LA MADIWANI KATIKA HALMASHAURI YA MANISPAA YA BUKOBA

 Mwenyekiti wa manispaa ya Bukoba , alexander Ngalinda akisikiliza kwa makini maelezo ya mkuu wa mkoa wa Kagera, John Mongella.
 Mkuu wa mkoa wa Kagera, Mongella kiongea na madiwani ya manispaa ya Bukoba, alikuwa akitoa ufafanuzi juu ya uamzi wa mkoa kujenga chuo cha VETA katika wilaya ya Bukoba  vijijini.
 Baadhi ya madiwani wakimsikiliza mkuu wa mkoa.
 Diwani wa kata ya Nshanbya,
 Baadhi ya wakuu wa idara katika manispaa ya Bukoba walioudhuria kikao hicho.
Mwenyekiti wa CHADEMA katika manispaa ya Bukoba, Victor Sherejei (kulia) na mkuu wa kituo cha polisi kati Halima.



Tuesday, February 17, 2015

WALIOFANYA UBADHILIFU WA UTEKELEZAJI WA MIRADI KATIKA MANISPAA YA BUKOBA KUKIONA CHA MOTO




 
NA AUDAX MUTIGANZI
BUKOBA
 
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kushirikiana na serikali kimeahidi kuwachukulia hatua kali za kisheria na kinidhamu viongozi wa kuchaguliwa na wananchi waliopewa jukumu la kusimamia   halmashauri ya manispaa ya BUKOBA  na baadhi ya watumishi waliofanya  ubadhilifu wa  fedha  zilizokuwa zimetengwa  kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo iliyokuwa imebuniwa katika manispaa hiyo .
 
Kauli hiyo imetolewa na NAPE NNAUYE,  katibu wa siasa itikadi na uenezi wa  taifa wa Chama Cha Mapinduzi CCM  kwenye hotuba yake aliyoitoa  kwenye maalumu mkutano wa hadhara ulifanyika kwenye uwanja wa uhuru wa kumsimika  DEONIZ MALINZI aliyeteuliwa kuwa kamanda wa jumuia ya  vijana  katika  mkoa wa KAGERA.
 
Sambamba na kauli hiyo, katibu huyo amemuagiza mkuu wa mkoa wa KAGERA , JOHN MONGELLA kuhakikisha anatafuta ufumbuzi  migogoro iliyochangia kukwamisha  miradi ya maendeleo katika manispaa hiyo iliyochangiwa na hatua ya baadhi ya  madiwani kugomea vikao vya baraza kwa zaidi ya miaka MIWILI jambo  lililodumaza maendeleo ya wananchi.
 

 
Katika mkutano huo Balozi KHAMIS KAGASHEKI  mbunge wa jimbo la BUKOBA mjini amenusha kwamba yeye sio chanzo cha migogoro iliyokwamisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo  katika manispaa hiyo bali yeye ni mtetezi wa wananchi, nao makada wa CCM,  AMIM  AHMED na PROTACE ISHENGOMA wanaeleza  namna chama hicho kilivyojipanga kuwawezesha vijana  kiuchumi huku wakiwahimiza  vijana kujiunga na vyama vya akiba na mikopo.
 

 
SADIK HASSAN ni mwenyekiti wa VIjana wa CCM wilaya ya NGARA anayewaleza vijana wajiepushe na udanganyifu unaofanywa na viongozi wa vyama vya upinzani  na kuwataka pia wasikubali kurubuniwa,  huku DIONIZ MALINZI kamanda wa vijana wa mkoa wa KAGERA akiahidi kuiimarisha jumuia ya vijana katika mkoa huo.
 

 
Mgogoro katika manispaa ya BUKOBA ulikwamisha utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo iliyokuwa imebuniwa ambayo ni pamoja na mradi wa ujenzi wa soko kuu la BUKOBA, upimaji wa viwanja ELFU tano, ujenzi wa standi kuu ya mabasi eneo la KYAKAILABWA na jingo la kitega uchumi.
 
Baadhi ya viongozi ambao ni madiwani wakiongozwa na BALOZI KAGASHEKI walipinga utekelezwaji wa miradi hiyo kwa madai kuwa ilikuwa imeghubikwa na vitendo vya ubadhilifu hali ambayo iliwagawa madiwani hadi baadhi yao wakafikia hatua ya kususia bikao.


Monday, February 16, 2015

PINDA AKAGUA DAWATI LA BEI NAFUU NA IMARA


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akikagua dawati  lenye ubora uliothibitishwa na Shirika la Viwango Tanzania lililouiniwa na kutengenezwa na Kampuni ya EDOSAMA HARDWARE ya jijini Dar es salaam, ofisini kwake Februari 16, 2015. Dawati hilo linalotengenezwa kwa mbao laini ambazo zimebanwa  bila kutumia misumari linakadiriwa kugharimu sh. 80,000/=. Wengine pichani  kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Eric Shigogo, Mkuu wa Idara ya Mikopo ya Benki ya TIB, Masanja Kungu, Ofisa Mazingira, Daniel Kapakala na Mkurugrnzi Msaidizi wa Kampuni hiyo,Edward Saguda. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)